EWE ROHO WA MBINGUNI

[1]
Ewe Roho wa Mbinguni, Maombi sikia!
Makao yako yafanye Mioyoni mwetu.

[2]
Kama nuru, tupenyeze, Giza uondoe;
Siri yako tuione, Na amani yako.

[3]
Kama moto, tusafishe, Choma dhambi yetu;
Roho zetu zote ziwe Hekalu la Bwana.

[4]
Kama umande, na uje, Utuburudishe,
Moyo `kavu utakuwa Ni wenye baraka.

[5]
Kama upepo Ee Roho, Katika Pente koste
Ukombozi utangaze, Kwa kila taifa.

04[2]