CHA KUTUMAINI SINA

[1]
Cha kutumaini sina ila damu yake Bwana,
Sina wema wa kutosha Dhambi zangu kuziosha.

Chorus
Kwake Yesu nasimama,
Ndiye mwamba: ni salama;
Ndiye mwamba: ni salama;

[2]
Njia yangu iwe ndefu yeye hunipa wokovu;
Mawimbi yakinipiga nguvuzake ndizo nanga.

[3]
Damu yake na sadaka nategemea daima,
Yote chini yakiisha Mwokozi atanitosha.

[4]
Nikiitwa hukumuni, Rohoni nina amani;
Nikivikwa haki yake sina hofu mbele zake.

06[9]