BWANA NI MCHUNGA

[1]
Bwana ni Mchunga, Sitahitaji;
Majani mabichi malisho yangu.
Ananinywesha maji matulivu;
Atanirudisha nikipotea.

[2]
Nipitapo bondeni mwa mauti
U mlinzi wangu sitaogopa;
Fimbo lako latosha kunilinda;
Ukinifariji sina hasara.

[3]
Kati ya mateso meza waandaa,
Na kikombe changu kinafurika;
Umenipaka kichwani mafuta;
Nitaulizaje zaidi kwako?

[4]
Wema na fadhili zinifuate
Siku zangu zote hata milele;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana
Katika ufalme wa pendo lake.

13[2]