BWANA NAMI

Language: Swahili
Nyimbo Za Kikristo

BWANA NAMI

[1]
Nimemwona rafiki wa thamani kubwa,
Ananipenda kwa ‘pole, kwa pendo amini:
Kuishi kute ngwa naye, la, huki siwezi,
Tunakaa pamoja: Bwana nami.

[2]
Pengine nimechoka, mimi mdhaifu,
Ndipo ninamtegemea, alivyoalika;
Huniongoza njiani, pahali pa nuru,
Twatembea pamoja: Bwana nami.

[3]
Namweleza huzuni, na fura ha yangu,
Vile ninavyosumbua, vinavyopendeza;
Huniagiza kutenda, yanayonipasa,
Twazungumza pamoja: Bwana nami.

[4]
Ajua natamani, kuwavuta watu,
Hivyo ananipeleka, kutangaza Neno;
Nitangaze pendo lak, kwa niniakafa;
Twahubiri pamoja: Bwana nami.

06[1]