BWANA, UNIONGOZE JUU

[1]
Nakaza mwendo mbinguni, kila siku napanda juu;
Naomba nikisafiri, ‘Bwana uniongoze juu.‘

Chorus
Bwana uniinue juu Kwa imani hata mbingu.
Juu kuliko dunia; Bwana uniongoze juu.

[2]
Moyo wangu hautaki Kukaa palipo shaka;
Wengine wapenda chini Nia yangu ni kupanda.

[3]
Nataka kupanda juu Nisishindwe na adui;
Kwa imani nasikia Sauti ya washindaji.

[4]
Kupanda juu nataka Niuone utukufu;
Hata mwisho nitaomba, ‘Bwana uniongoze juu.‘

07[3]