ATI, KUNA MVUA NJEMA

[1]
Ati, kuna mvua njema yenye neema;
Watu wanaona vyema Bwana, huninyeshei?

Chorus
Na mimi? Na mimi? Bwana, huninyeshei?

[2]
Sinipite, Baba mwema; dhambini nimezama:
Rehema ni za daima; Bwana hunionyeshi?

[3]
Sinipite, Yesu mwema; niwe nawe daima,
Natamani kukwandama: Bwana, hunichukui?

[4]
Sinipite, Roho mwema, Mpaji wa uzima,
Nawe shahidi wa wema, Bwana wema hunipi?

03[9]