ANAKUJA BWANA YESU

Song Lyrics

ANAKUJA BWANA YESU

Nyimbo Za Kikristo · Swahili
Present

Lyrics

Font size:
[1]
Pengine ni saa ya kupambazuka,
Mishale ya jua ipenyapo giza,
Kwamba atakuja Yesu mtukufu,
Awapokee wake.

Bwana itakuwa lini Tutapoimba,
‘Anakuja, Bwana Yesu, Aleluya,
Amin, Aleluya, Amin?‘

[2]
Pengine mchana, pengine jioni,
Pengine usiku wa manane, giza,
Itatoweka kwa fahari akija,
Awapokee wake.

[3]
Majeshi yake yataimba ‘Hosana,‘
Na watakatifu waliotukuzwa,
Watamsifu kwa kuwa amekuja,
Awapokee wake.

[4]
Furaha tukiitwa pasipo kufa,
Pasipo kuona maradhi, machozi;
Kuchukuliwa winguni kwa fahari,
Akija kwa watu wake.

16[3]

Support My Songbooks

Help us expand our library and keep the music alive for everyone. Even a small donation goes a long way.

Buy me a coffeeBuy us a coffee