ubujiko

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

ubujiko

[1]
Damu imebubujika, Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli.

[2]
Ilimpa kushukuru Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.

[3]
Kondo-o wa kuuawa, Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa kwa utimilivu.

[4]
Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako. ‘taimba milele.

[5]
Bwana, umenikirimu Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.

[6]
Nikubali kumwimbia Mbinguni milele.
Mungu nitamsifia Jina lako pweke.