subuhi

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

subuhi

[1]
Bwana asubuhi kucha nitakuinua
Sauti yangu kuomba, nipate baraka.

[2]
Nakuomba roho yako niongozwe nayo;
Nifanye yanipasayo, na mapenzi yako.

[3]
Wanaokutegemea, U Mlinzi wao;
Matumaini wanayo, utayatimiza.

[4]
Na kwa wingi wa fadhili, Nyumbani mwako juu
Nitaingia na wimbo, Pale kusujudu.