Mungu

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Mungu

[1]
Nena rohoni Yesu, Nena kwa upole
Sema kwangu kwa pendo, “Huachwi upweke.”
Fungua moyo wangu, Nisikie mara;
Jaza roho na sifa, Sifa zako Bwana.

Kila siku unene, Vile kwa upole,
Nong‘oneza kwa pole wa pendo:
“Daima utashinda, Uhuru niwako.”
Nisikie maneno: “Huachwi upweke.”

[2]
Nena kwa wana wako, Waonyeshe njia,
Wajaze kwa furaha, Fundisha kuomba;
Wajifunze kutoa Maisha kamili,
Wahimize ufalme, Tumwone mwokozi.

[3]
Nena kama zamani, Ulipoitoa
Sheria takatifu: Niiweke pia;
Nipate kutukuza Wewe Mungu wangu,
Mapenzi yako tena, Daima kusifu.

[4]
Kila siku unene, Vile kwa upole.
Nong‘oneza kwa pole wa upendo:
“Daima utashinda, Uhuru ni wako.”
Nisikie maneno: “Huachwi upweke.”