sinipite

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

sinipite

[1]
Usinipite, Mwokozi, unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.

Bwana, Bwana, Unisikie;
Unapozuru wengine, usinipite.

[2]
Kiti chako cha rehema, nakitazama;
Magoti napiga pale, nisamehewe.

[3]
Sina ya kutegemea, ila wewe tu;
Uso wako uwe kwangu: nakuabudu.

[4]
Wewe tu u mfariji: sina mbinguni,
Wala duniani pote, Bwana mwingine.