Shani Ya Mungu

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Shani Ya Mungu

[1]
Nasifu shani ya Mungu, mweneza bahari,
Muumba pia wa mbingu, Jua, Nyota, mwezi,
Ni tukufu yaki shani, mtengeza mambo
Ya nyakati na zamani, yasiyo na mwisho.

[2]
Kadiri ya nionayo, ya kusifu Mungu:
Nchi niikanyagayo, na hayo mawingu;
Hakuna hata unyasi, usiokukuza;
Na upepo wavumisha, au kutuliza.

[3]
Nami kwa mkono wako, naongozwa sawa,
Ni pato nikusifupo, kukwomba ni dawa;
Umenizingira nyuma, na mbele baraka,
Maarifa ya ajabu! Yanishinda mimi!