Sauti Yako

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Sauti Yako

[1]
Nasikia mwito, Ni sauti yako;
Nikasafiwe kwa damu Ya kwangikwa kwako.

Nimesongea mtini pako,
Unisafi kwa damu ya kwangikwa kwako.

[2]
Ni mnyonge kweli, umenipa nguvu;
Ulivyonisfi taka Ni utimilivu.

[3]
Yesu hunijuvya: Mapenzi imani,
Tumai, amani, rahi, hapa na mbinguni.

[4]
Napata wokovu, Wema na neema;
Kwako Bwana nina nguvu Na haki daima.