Rohoni Mwangu

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Rohoni Mwangu

[1]
Nionapo amani kama shwari, au nionapo shida;
Kwa hali zote umenijulisha ni salama rohoni mwangu.

Salama rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

[2]
Ingawa Shetani atanitesa, nitajipa moyo kwani,
Kristo ameona unyonge mwangu; amekufa kwa roho yangu.

[3]
Dhambi zangu zote, wala si nusu, huwekwa msalabani;
Wala sichukui laana yake, ni salama rohoni mwangu.

[4]
Ee Bwana himiza siku ya kuja, panda itakapolia:
Utakaposhuka sitaogopa ni salama rohoni mwangu.