Ni Mchunga

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Ni Mchunga

[1]
Bwana ni Mchunga, Sitahiji;
Majani mabichi malisho yangu.
Ananinywesha maji Matulivu;
Atanirudisha nikipotea.

[2]
Nipitapo bondeni mwa mauti
U mlinzi wangu—sitaogopa;
Fimbo lako latoshakunilinda;
Ukinifariji sina hasara.

[3]
Kati ya mateso mea waandaa,
Na kikombe changu kinafurika;
Umenipaka kichwani mafuta;
Nitaulizaje zaidi kwako?

[4]
Wema na fadhili zinifuate
Siku zangu zote hata milele;
Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana
Katika ufalme wa pendo lake.