Nawe Nanyi Daima

[1]
Mungu nawe nanyi daima; hata twonane ya pili,
Awachunge kwa fadhili, Mungu nawe nanyi daima.

Hata twonane juu, hata twonane tena kwake;
Hata twonane juu, Mungu nawe nanyi daima.

[2]
Mungu nawe nanyi daima; awafunike mabawa,
Awalishe, awakuze; Mungu nawe nanyi daima.

[3]
Mungu nawe nanyi daima; kila wakati wa shida
Awalinde hifadhini; Mungu nawe nanyi daima.

[4]
Mungu nawe nanyi daima; awabariki na pendo
Ambalo halina mwisho; Mungu nawe nanyi daima.