Nami

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Nami

[1]
Kaa nami, ni isiku tena;
Usiniache gizani, Bwana.
Msaada wako haukomi;
Nili peke yangu, kaa nami.

[2]
Siku zetu hazakawi kwisha;
Sioni la kunifurahisha;
Hakuna ambacho kakikomi,
Isiye na mwisho kaa nami.

[3]
Nina haja nawe kila saa;
Sina mwingine wa kunifaa
Mimi nitaongozwa na nani
Ila wewe? Bwana, kaa nami.

[4]
Sichi neno uwapo karibu;
Nipatalo lote si taabu;
Kifo na kaburi haviumi;
Nitashinda kwako, kaa nami.

[5]
Nilalapo nikuone wewe,
Gizani mote nimulikiwe;
Nuru za mbinguni hazikomi,
Siku zangu zote; kaa nami.