Lako, Ee Mwikozi

[1]
Pendo lako, Ee Mwokozi, Hushinda pendo zote!
Kaa nasi, ndani yetu, furaha ya mbinguni.
Yesu, u rehema tupu. Safi na kusamehe,
Mfariji mwenye huzuni Ziondoe machozi.

[2]
Roho yako ya upendo Tuma kwa kundi lako;
Hebu tuirithi raha, iliyoahidiwa.
Uondoe moyo mbaya, U Mwanzo, tena Mwisho
Timiza imani yetu, Ili tuwekwe ‘huru.

[3]
Yesu, uje kwetu sasa, Tupokee huruma;
Rudi kwetu, tena kamwe Usituache pekee.
Tungekutukuza leo, Pamoja ma malaika,
Imba na kutoa sifa, Ingia kwa ibada.

[4]
Sasa, Bwana, kazi yako, Imalize moyoni;
Takasa hekalu lako, wokovu kamilisha!
Safisha viumbe vyako Katika wakati huu:
Tupumzike ‘toka dhambi, Tuingie mbinguni.