Kama Mchunga

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Kama Mchunga

[1]
Mwokozi, kama mchunga
Utuongoze leo;
Ututume malishoni;
Fanya tayari boma.
Bwana Yesu, peke yako
Umetuvuta kwako.

[2]
Tu wako, uwe rafiki,
Uwe mlinzi wetu;
Kundi lako ulilinde,
Tusivutwe na dhambi;
Bwana Yesu, tusikie,
Tukiomba, samehe.

[3]
Umetuahidi kwamba
Utakubali watu;
Utawahurumia na
Utawapa neema;
Bwana Yesu, tunapenda
Kuwa wako, mapema.