Imara, Ninyi Wa Bwana

[1]
Msingi imara, ninyi wa Bwana,
Ume wekwa kwenu kwa neno lake?
Nini zaidi atasema Bwana?
Imani yenu ipate kuzidi?

[2]
Wambiwapo vuka maji ya giza,
Mito ya mashaka haitazidi;
‘Takuwapo nawe, nikuwezeshe,
Shida upatazo zisikutishe!

[3]
Utakapopishwa Ndani ya moto
Nguvu nitakupa, upate pato;
Huteketezwi, ila taka zako.
Na zitasalia dhahabu zako.

[4]
Na mtu aliyenitegemea
Nguvu za jehanamu zijapotisha,
Kamwe kwa adui sitamtia;
Mtu wangu kamwe sitamuacha.