Hukumuni?

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Hukumuni?

[1]
Hapo Yesu atakapoita mataifa mbele yake,
Tutashindaje kwenye hukumu mbele ya kiti cha enzi?

Atakusanya ngano ghalani, atatupambali makapo;
Tutashindaje hukumuni siku kuu ya kiyama?

[2]
Je, tutasikua neno tamu: “vema, wewe mtumwa mwema,”
Ama wenye uchunguna hofu tutakatazwa ufalme?

[3]
Atakubali tu kwa furaha watoto wake wapendwa,
Atawapa mavazi meupe, wakea tayari kumlaki.

[4]
Hivyo tukeshe, nasi tungoje, wenye taa zinazo waka;
Tutakapoitwa arusini tuwe tayari kumlaki.

[5]
Roho ikielekea mbingu twangoja wenye saburi,
Hata safari yetu iishe, tukae kwake milele.