Hai, Yu Hai

Language: Swahili
Nyimbo za Kristo

Hai, Yu Hai

[1]
Yesu Bwana Mwokozi aishi milele,
Najua kwamba Yupo pamoja na mimi;
Sauti nasikia, Rehema naona;
Wakati namhitaji, yupo nami.

Yu hai, Yu hai,Yu hai Bwana Yesu!
Atembea, azungumza nami siku zote.
Yu hai, Yu hai, kutoa uzima!
Hivi ndivyo nijuavyo,
Yu hai ndani yangu!

[2]
Ulinzi Wake upo naona dhahiri,
Miguu ichokapo, sikati tamaa.
Najua an‘ongoza kupota dhoruba,
Siku ya kuja kwake nitamwona.