Jiwe Kuu La Pembeni

[1]
Mungu ni Baba wetu
Ndiye Muumba vyote
Uwezo na ushindi
Hupatikana kwake.

[chorus]
Bwana Mungu asema
Tazama naliweka
Jiwe kuu la pembeni
Lililo jaribiwa

[2]
Bwana wetu ni Kristo
Ndiye mwamba wa pekee
Jiwe kuu la pembeni
Liliwekwa na Mungu

[chorus]
Bwana Mungu asema
Tazama naliweka
Jiwe kuu la pembeni
Lililo jaribiwa

[3]
Yesu alilijenga
Kanisa juu ya mwamba
Milango ya kuzimu
Haiwezi kushinda.

[chorus]
Bwana Mungu asema
Tazama naliweka
Jiwe kuu la pembeni
Lililo jaribiwa

[4]
Naye Yesu ni kichwa
Ni kichwa cha kanisa
Naye ni mzaliwa
Wa kwanza toka wafu

[chorus]
Bwana Mungu asema
Tazama naliweka
Jiwe kuu la pembeni
Lililo jaribiwa

[5]
Mungu Baba atukuzwe
Baba na Bwana Yesu
Aliyetubariki
Baraka za rohoni.

[chorus]
Bwana Mungu asema
Tazama naliweka
Jiwe kuu la pembeni
Lililo jaribiwa