HUZUNI NYINGI

Language: Swahili
Nyimbo Za Umoja

HUZUNI NYINGI

[1]
Huzuni nyingi kwa sisi wote (washiriki).
Kuagana e ndugu,
Tulikuwa pete na kidole (nanyi ndugu)

[chorus]
Kwa heri e ndugu.
Kwa heri e ndugu,
Kwa heri e ndugu,
Kwa heri, kwa heri (ndugu zetu).
Tutajaonana Mwenyezi (akipenda)
Enenda kwa amani,
Kwa heri (ndugu zetu).

[2]
Mmeacha pengo kubwa sana (kwetu sisi)
Pete na kidole,
Mungu awe nanyi katika safari (yenu)
Kwa heri e ndugu.

[3]
Tukumbukane ndugu kwa njia ya (maombi)
Kwa heri e ndugu,
Jina la Yesu ni ngome yetu (sisi sote)
Kwa heri e ndugu.