BWANA YESU ALISEMA

[1]
Bwana Yesu alisema, Ufalme wa Mbinguni,
Ni sawa na mkulima, aliyeajiri watu,
Wa mtumikie katika shamba la mizabibu. x2

Ali-ajiri asubuhi, ali-ajiri na saa tatu
Ali-ajiri na mchana, ali-ajiri na saa tisa;
Ali-ajiri na jioni “wote” walipata dinari.
Walioanza asubuhi, “wote,” walilalamika sana
Kwa nini unatulinganisha, “na sisi” na wale wa jioni?
“Tuli” patanaje na ninyi?
“Tuli” patana mpewe dinari, x2
“Ndugu” dinari ni uzima,
“Kweli tutapata uzima. x2

[2]
Mungu hachagui mtu, wala kumpendelea,
Tajiri na maskini, kwake Mungu wote sawa
Na mshahara wa wote ni uzima wa milele. x2