JINA LANGU LIMEANDIKWA JE

[1]
Sitafuti mali, wala utajiri; Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu, Jina langu yakini limeandikwa, je?

Chorus
Limeandikwa, je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa, je?

[2]
Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga, Lakini damu yako, Mwokozi, yatosha;
Kwani umeahidi: zijapo nyekundu Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.

[3]
Mji mzuri sana, wa majumba makuu, Walipo malaika, mji bila ovu;
Wakaapo walio na mavazi safi, Limeandikwa sasa, jina langu huko?

170