BUBUJIKO

Song Lyrics

BUBUJIKO

Nyimbo Za Kikristo · Swahili
Present

Lyrics

Font size:
[1]
Damu imebubujika, Ni ya Imanweli,
Wakioga wenye taka, Husafiwa kweli.

[2]
Ilimpa kushukuru Mwivi mautini;
Nami nisiye udhuru, Yanisafi ndani.

[3]
Kondo-o wa kuuawa, Damu ina nguvu,
Wako wote kuokoa Kwa utimilivu.

[4]
Bwana, tangu damu yako Kunisafi kale,
Nimeimba sifa zako, `taimba milele.

[5]
Bwana, umenikirimu Nisiyestahili
Kwa damu yako, sehemu Ya mali ya kweli.

[6]
Nikubali kukwimbia Mbinguni milele.
Mungu nitamsifia Jina lako pweke.

11[3]


Support My Songbooks

Help us expand our library and keep the music alive for everyone. Even a small donation goes a long way.

Buy me a coffeeBuy us a coffee